Home » » MISAADA ZAIDI YAENDELEA KUTOLEWA KWA MTOTO ALIYEFUNGIWA NDANI MIAKA MIWILI.

MISAADA ZAIDI YAENDELEA KUTOLEWA KWA MTOTO ALIYEFUNGIWA NDANI MIAKA MIWILI.

 Christian Mwakapusya Mtanzania anaeishi Marekani  akiwa amembeba mtoto Joshua Joseph baada ya kumtembelea nyumbani kwao Iyunga Jijini Mbeya

 David Mwakapusya ambaye alifuatana na Baba yake akitoa msaada wa nguo kwa mtoto ambaye hakufahamika jina lake kwa niaba ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu mtaani hapo.
 Baadhi ya Majirani wa familia ya Joshua wakiwa na nguo walizopewa na Christian Mwakapusya
 Christian Mwakapusya akizungumza na mama mlezi wa mtoto Joshua Joseph Nyumbani kwake Iyunga Jijini Mbeya.

Christian Mwakapusya akizungumza na Amina Mwasankinga aliye simamishwa masomo kwa kisingizio cha ushirikina alipo kutana nae katika Ofisi za Mbeya yetu.
******************

MTANZANIA anayeishi Marekani Christian Mwakapusya aliyeguswa na kitendo alichofanyiwa  mtoto mwenye umri wa zaidi ya miaka miwili kufungiwa ndani na wazazi wake kwa kipindi cha miaka miwili sasa bila kutoka nje pamoja na kukosa matunzo muhimu hali ambayo imepelekea mtoto huyo kudhoofu kiafya.

Kutokana na kuguswa na tukio hilo Mtanzania huyo amelazimika kumtembelea Nyumbani anakoishia na kujionea hali halisi aliyonayo mtoto huyo kwa sasa.

Akizungumza kwa masikitiko nyumbani kwao eneo la Iyunga Mwakapusya amesema Wazazi wanaofanya vitendo kama hivyo wanapaswa kulaaniwa na kukemewa.

Mwakapusya aliyekuwa amefuatana na Mtoto wake wa Kiume David waliofunga safari kutoka Marekani hadi Mbeya kumwona Mtoto huyo wametoa zawadi mbali mbali zikiwemo Nguo na fedha taslimu alizokabidhiwa Mama mlezi pamoja na Balozi wa Nyumba kumi.

Mhanga wa tukio hilo, Joshua Joseph umri unao kadiriwa  kuwa ni kati ya miaka miwili au mitatu  ambaye alikutwa nyumbani hapo akiwa pekee yake huku wazazi wake wakiwa wameondoka kuelekea kwenye shughuli zao .

Balozi wa mtaa huo wa Ikuti Ndugu Aloni Mboya amesema kuwa hali hiyo imenza kujitokeza kwa kipindi cha miaka mitatu sasa hali ambayo imepelekea mtoto huyo kukumbwa na maradhi ya utapiamlo.

Amesema katika kipindi cha mwaka 2011 mwezi wa tatu alipokea  taarifa kuhusiana na   suala hilo  ambapo baba wa mtoto huyo ndugu Joseph Simoni aliitwa katika ofisi za mtaakwa lengo la kumhoji juu ya malezi ya mtoto huyo.

Wakati huo huo Msamaria mwema huyo kutoka Nchini Marekani pia amezungumza na Mwanafunzi mwenye ulemavu wa ngozi (albino) Amina Mwasankinga ambaye alifukuzwa Shule kwa kisingizio cha Ushirikina.

Aidha amemuahidi kumsaidia ili aweze kumaliza masomo yake huku akilaani vikali kitendo cha Walimu wa Shule ya Hollwood ya Wilayani Mbozi kuamini imani za Kishirikina na kumharibia masomo Mwanafunzi huyo.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Sweet Home - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger